Vijana kutoka Uingereza wapo "gado" kumsubiri Papa Francisko!
Ujumbe wa vijana 800 kutoka Uingereza unaoongozwa na Maaskofu 5 umewasili mjini Rio
de Janeiro, tayari kushiriki katika Maadhimisho ya Siku ya 28 ya Vijana Duniani kwa
mwaka 2013. Baba Mtakatifu Francisko anatarajiwa kuwasili nchini Brazil, jumatatu
jioni. Vijana hawa wamejiandaa kiroho na kimwili ili kushiriki katika Maadhimisho
haya ambayo ni hija ya maisha ya kiroho.
Taarifa inaonesha kwamba, kuna idadi
kubwa pia ya waandishi wa habari kutoka Uingereza wanaoshiriki katika Maadhimisho
ya Siku ya Vijana Duniani. Vijana wanaalikwa na Baba Mtakatifu Francisko kuwa ni Wainjilishaji
wa vijana wenzao katika mitandao ya kijamii.