2013-07-20 14:10:13

Kardinali Simoni Ignatius Pimenta afariki dunia!


Baba Mtakatifu Francisko ametuma salam za rambi rambi kwa Jimbo kuu la Bombay, India kutokana na kifo cha Kardinali Simon Ignatius Pimenta, Askofu mkuu mstaafu wa Jimbo kuu la Bombay. Baba Mtakatifu anamkumbuka kwa namna ya pekee Marehemu Kardinali Pimenta kutokana na majitoleo yake kwa Kanisa na uaminifu mkubwa aliouonesha kwa Khalifa wa Mtakatifu Petro enzi ya uhai wake.

Baba Mtakatifu anaungana na Familia ya Mungu, Jimbo kuu la Bombay kwa ajili ya kumwombea Marehemu kardinali Pimenta, ili roho yake iweze kupata pumziko la milele. Baba Mtakatifu anatoa baraka zake za kichungaji kwa wale wote watakaoshiriki katika Ibada ya Mazishi ya Kardinali Simoni Ignatius Pimenta.







All the contents on this site are copyrighted ©.