Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Afrika na Madagascar katika mkutano wake
mkuu wa kumi na sita uliofunguliwa na Kardinali Polycarp Pengo, Rais wa SECAM aliyemaliza
muda wake, umewachagua viongozi wafuatao:
Askofu mkuu Gabriel Mbilingi wa Jimbo
kuu la Lubango, Angola, Rais wa SECAM.
Askofu Louis Portella Mbuyu wa Jimbo
la Kinkala, Congo Brazzaville, Makamu wa Rais SECAM.
Askofu mkuu Anokye wa
Jimbo kuu la Kumasi, Ghana, Makamu wa Pili wa Rais SECAM.
Mheshimiwa Padre
Joseph Komakoma kutoka Zambia, Katibu mkuu wa SECAM.
Mheshimiwa Padre Père
Samuel de Jesus Paquete, kutoka Angola, Katibu mkuu Mwambata wa SECAM.