Simameni kidete kulinda na kutetea haki msingi za binadamu kama njia ya kumuenzi Mzee
Madiba
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki-Moon ametuma salam na matashi mema kwa
Mzee Nelson Mandela ambaye tarehe 17 Julai 2013 ameadhimisha Miaka 95 tangu alipozaliwa.
Maadhimisho haya yanapaswa kuwa ni kikolezo cha ujenzi wa mshikamano na huduma kwa
wengine; kwa kusimama kidete kulinda na kutetea haki msingi za binadamu kama alivyofanya
Mzee Madiba.
Jumuiya ya Kimataifa anasema Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa
inapaswa kutenda sanjari na kuibua mawazo yatakayoleta mabadiliko katika mchakato
wa ujenzi wa dunia yenye amani, usawa na maendeleo endelevu kama njia ya kumuenzi
Mzee Madiba aliyefanikiwa kumwilisha ndani mwake fadhila mbali mbali za kibinadamu
na kiutu.