Mzee Nelsona Mandela ambaye amelazwa Hospitalini kutokana na hali yake kudhohofu,
wakati wowote kuanzia sasa anaweza kutolewa Hospitalini na kurudishwa nyumbani ili
kuendelea na matibabu akiwa nyumbani kwake.
Hayo yamesemwa na Rais mstaafu
Thabo Mbeki wa Afrika ya Kusini, mwishoni mwa Juma, katika hotuba yake kama kumbu
kumbu ya mchango wa Mzee Madiba, katika mkutano mkuu wa Chama cha Ukombozi cha Afrika
ya Kusini, ANC. Wachunguzi wa mambo wanasema, kwa hakika Mzee Madiba "amekuwa ngangari
hata kwa kifo".
Alikaa kifungoni kwa miaka 27 na kunako mwaka 1994 akachaguliwa
kuwa Rais wa Afrika ya Kusini na kung'atuka madarakani kunako mwaka 1999. Thabo Mbeki
akarithi kigoda cha Mzee Madiba.