2013-07-11 08:48:13

Adhabu ya kifo, ni kinyume cha haki msingi za binadamu!


Jumuiya ya Mtakatifu Egidio yanye Makao yake Makuu mjini Roma, imekuwa mstari wa mbele kuihamasisha Jumuiya ya Kimataifa kufuta adhabu ya kifo kwani adhabu hii ni kinyume cha haki msingi za binadamu na badala yake kuangalia uwezekano wa kutoa adhabu mbadala. RealAudioMP3

Hadi sasa kuna mafanikio makubwa yaliyokwisha kupatikana kutokana na harakati hizi, lakini bado Jamii inapaswa kufundishwa ili kutambua kwamba, haki, amani, msamaha na upendo ni fadhila fungamanishi. Adhabu ya kifo haimtendei haki mtuhumiwa. Ni maneno ya MS Queen Said, Mratibu wa Jumuiya ya Mtakatifu Egidio nchini Tanzania katika mahojiano maalum na Radio Vatican. Anasema, Jamii inapaswa kutambua athari za adhabu ya kifo, ili kusimama kidete kulinda na kutetea uhai ambayo ni zawadi kubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu.







All the contents on this site are copyrighted ©.