2013-07-06 15:30:23

Waraka wa kwanza wa Papa Francisko:Mwanga wa Imani


Waraka wa kwanza wa Kichungaji wa Papa Francisko wenye jina: Mwanga wa Imani, "Lumen Fidei" ulitolewa Ijumaa katika mkutano wa waandishi wa habari. Waraka huo unakamilisha mafundisho ya kipapa juu fadhila za Kimungu; yaani: Imani, Matumaini na Mapendo, yaliyoanzishwa na Papa mstaafu Benedikto XVI, kwa kutoa nyaraka mbili juu ya Mungu ni Upendo "Deus Caritas Est" mwaka 2005 na Tumaini Linalookoa "SPE Salvi" mwaka 2007.

Papa Fransisiko awali, akitangaza juu ya waraka wake wa kwanza wa kichungaji , Mwanga wa Imani alileleza kwamba , waraka huo ni kazi ya iliyoanzishwa na Mtangulizi wake Papa mstaafu Benedikto XVI, ambaye aliipitisha rasimu yake kwa ajili ya Papa mpya kuikamilisha. Na kwamba ni wazi waraka huo , umeendeleza mandhari nyingi zilizo mpendeza Papa mstaafu Benedikto XVI ikisaidiwa na msaada kutoka hati ingine ya imani na hoja, hadi katika furaha binafsi ya kukutana na Kristu. Na katika maadhimisho ya Mwaka wa Imani miaka 50 ya Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican , waraka unalenga kuhamasisha mwamko mpya wa kiini cha wajibu wa imani katika moyo wa mahusiano yote ya binadamu.

Waraka mpya uliotolewa umetengwa katika sura nne, zinazotanguliwa na utangulizi mfupi. Waraka huo unalenga kuonyesha jinsi imani katika Yesu Mfufuka inavyoweza kumwongoza Muumini kuona zaidi ya mipaka ya upeo finyu unaomfungia mtu binafsi, nje ya jamii zima katika umoja wa upendo wa Mungu. Dhana ya upofu wa imani, wenye kuzuia maendeleo ya kisayansi na kumfanya mtu kubaki katika gizani, na kinyume chake muumini huigundua sauti inayomwita kuuona mwanga unaoweza kuwaongoza watu wote kutoka giza la ubinafsi kuelekea ukweli zaidi na dunia ya udugu , iliyosimikwa katika ahadi za Mungu Muumba.
Sura ya kwanza inampeleka msomaji, katika Agano la Kale na Agano jipya , tangu wakati wa Abrahamu , aliyeisikia sauti ya Mungu ikimwita hadi wakti Waisrael wakisafiri kuelekea mwanga wa Nchi ya Ahadi , hadi kwa kifo cha Yesu Msalabani, Kipeo cha Upendo wa Mungu kwa binadamu. Katika sura hii ujumbe wa Papa, unatazamisha katika kuguswa na nguvu ya upendo katika kufanya mageuzi. ikilenga kutupa mwanga zaidi katika kuelewa mahusiano yetu na ndugu zetu katika Kristu, wake kwa waume.

Sura Pili, inasisitiza juu ya kiungo muhimu kati ya Imani na Ukweli, ambavyo bila hivyo imani inaonekana kuwa si kitu zaidi ya hadhithi za kufikirika na furaha za mpito zisizo weza kutudumisha wakati wa majaribu magumu. Katika jamii ya sasa , Waraka mpya unasema , kuna mwelekeo wa kuyaona maendeleo ya teknolojia na furaha ya mtu binafsi, kuwa ndiyo ukweli msingi, katika mtazamo mpana juu ya masuala ya uwepo wa asili yetu kama mashaka makubwa.
Bila ya upendo katika mioyo yetu , ukweli huwa baridi, na huonekana kama kitu binafsi na ukandamizaji usioweza kuyabadilisha maisha ya watu wengine. Lakini kwa kusikiliza , kuona na kuamini uwepo wa Kristu katika maisha yetu ya kila siku, tunaweza kupanua mipaka yetu ya kuona mbali zaidi na hivyo kuwa na njia zilizo bora zaidi katika kutmikia kwa ajili ya mazuri ya wote. Mwanga wa Imani Yetu katika Kristu , unaweza kutoa mchango mkubwa katika ufanikishaji wa matunda ya majadiliano na wasiokuwa Wakristu na wasioamini Mungu, ukionyesha jisi wale wanaomtafuta Mungu au kuutafut ukweli wanavyokaribinswa na kumulikiwa na Mwanga huo.

Sura ya Tatu , imesimikwa juu ya Kanisa kama mahali ambapo mwanga wa imani unalindwa na kuenezwa kiazazi hadi kizazi. Kupitia Sakramenti ya Ubatizo na Ekaristi, kupitia kukiri Imani, sala kwa Baba Yetu na kutii amri za Mungu, Kanis ahufundisha lugha ya imani na kutuleta sisi katika upendo wa Utaatu Mtakasifu ili kwamba kila anayeamini si mpweke.
Na sura ya nne na ya mwisho, inalenga katika Imani na mazuri kwa wote, na kuonyesha jinsi mwanga wa imani unavyoweza kukuza amani na maridhiano , na kufundisha heshima katika uumbaji wa Mungu. Waraka pia unazingatia maeneo yanayomulikiwa na mwanga huo, tangu familia iliyosimikwa katika msingi ya ndoa na maelewano kama muungano thabtiti kati ya mwanaume na mwanamke. Imani anaandika Papa, haiwezi kufuta mateso duniani , lakini hutusindikiza katika kukabiliana nayo na pia hutupatia tumaini jipya katika upendo wa Mungu. Waraka huo unakamilika na Sala kwa Bikira Maria, Mama wa Yesu, mfano wa Imani, mwenye kutuongoza sisi katika kuuona Mwanga wa upendo wa Mungu.








All the contents on this site are copyrighted ©.