Ndugu na Jamaa ya Mzee Nelson Mandela wanasema kwamba, hali ya Mzee Madiba inazidi
kuwa mbaya siku hadi siku na kwa sasa anapumua kwa kusaidiwa na mashini. Wakati wowote
madaktari wake wataweza kutoa taarifa rasmi kuhusu maendeleo ya Mzee Madiba ambaye
kwa wiki tatu hivi mshumaa wa maisha yake unaendelea kupambana na mawimbi makali.
Wananchi wa Afrika ya Kusini na wapenda amani kutoka sehemu mbali mbali za
dunia wanaendelea kuimba, kusali na kukesha kwa ajili ya Mzee Madiba, wakiyaweka maisha
yake mikononi mwa Mwenyezi Mungu.