2013-07-04 14:56:17

Mamlaka ya Usalama wa Fedha Vatican yajiunga na Mtandao wa fedha wa Kimataifa


Mamlaka ya Usalama wa Fedha Vatican, ( Vatican Financial Intelligence Authority (AIF) imekubaliwa kujiunga katika mtandao wa kimataifa wa wa Kikundi cha Egmont, ambacho huunganisha Vitengo vya Usalama wa Fedha (Units Financial Intelligence (FIU)) katika ngazi ya kimataifa.

Katika Mkutano wake Mkuu wa 21, uliofanyika Sun City Afrika Kusini, kikundi cha Egmon, kilikubali kuuingiza AIF ya Vatikan kama mwanachama kamili.

Wanachama wa kikundi cha Egmont, huhakikisha uwepo upatikanaji wa misaada katika mtandao wa kimataifa wa FIUs na wenye kuwezesha kubadilishana habari katika mapambano dhidi ya uhalifu wa kifedha. Hatua hii kwa Jimbo la Papa na jijji la Vatican, ni alama ya hatua mbele zaidi, katika mchango wake kwenye juhudi za kimataifa, kupambana na uhalifu wa kifedha. .

Kusajiriwa kwa AIF katika kundi la Egmont, kunaonyesha kutambuliwa kwa Jimbo la Papa na Jiji la Vatican , katika utaratibu wa kufuatilia na kupambana na fedha inayotolewa haramu kufadhili ugaidi, ameleeza René Brülhart, Mkurugenzi wa AIF ". Na kwamba kusajiriwa kwa AIF katika mtandao huu wa kimataifa, kuna boresha zaidi uwezo wao , katika kuchangia kwenye mapambano ya ughaidi na uhalifu wa kifedha.

Kundi Egmont lilianzishwa mwaka 1995 na sasa wanachama ( FIUs) zaidi ya 130 za kitaifa. Ni jukwaa la FIUs duniani kote na katika kubadilishana habari na kuratibu mapambano dhidi ya fedha haramu na ufadhili wa ugaidi.








All the contents on this site are copyrighted ©.