Rais Barack Obama wa Marekani na Rais Mstaafu George W. Bush wa Marekani kwa pamoja,
Jumanne tarehe 2 Julai 2013 wameshiriki katika kumbu kumbu ya watu waliofariki dunia
wakati Ubalozi wa Marekani Jijini Dar es Salaam ulipolipuliwa kwa bomu kunako mwaka
1998.
Wachunguzi wa mambo wanasema, haya ni matukio machache sana ambayo Marais
hawa wawili wameonekana kwa pamoja hadharani. Wameweka shada la maua na baadaye kushikana
mikono na ndugu na jamaa ya wale walioathirika kutokana na mlipuko huo. Rais mstaafu
George W. Bush yuko Jijini Dar es Salaam ili kushiriki mkutano wa wanawake ulioandaliwa
na Taasisi ya Bush katika mchakato wa kuwajengea uwezo wanawake Barani Afrika.