2013-07-01 16:53:03

Papa kukitembelea kisiwa cha Lampedusa Italy


Jumatatu ya tarehe 8 Juli 2013, Papa Fransisko, atafanya ziara ya nusu siku katika kisiwa cha Lampedusa Italy.
Taarifa zinasema, ,akiwa ameguswa na taarifa ya kuzama kwa mashua iliyokuwa imebeba wahamiaji na wakimbizi waliolenga kuingia Italy bila kibali, hivi karibuni, wahamiaji kutoka Afrika, ikiwa moja ya matukio ya namna hiyo mfululizo, Papa anania ya kwenda kuwaombea wale wote waliopoteza maisha yao baharini , na pia kukutana na waathirika na wakimbizi waliopo sasa katika kisiwa hicho.
Pia anakwenda kuonyesha mshikamano wake na watu wa kisiwa hicho na kuhimiza uongozi na wote wenye mamlaka kuwajibika zaidi, kwa ajili ya kuhakikisha kwamba, huduma nzuri ni zinatolewa kwa watu wakimbizi na wahamiaji hao , wake kwa waume, ambao sasa wanaishi wako katika shida na mahangaiko makubwa.








All the contents on this site are copyrighted ©.