2013-07-01 16:35:23

Papa Fransisko asema: sala inahitaji kuwa jasiri na kung'ang'ana


Tunapaswa kuomba kwa ujasiri kwa Bwana, na kung'ng'ania kama alivyofanya Abrahamu. Ni himizo lililotolewa na Papa Fransisko , mapema Jumatatu hii wakati wa Ibada ya Misa, aliyo iongoza katika Kanisa ndogo la Mtakatifu Marta, hapa Vatican. ambamo alielezea juu ya kuomba, kwamba ni kufanya mazungumzo na Bwana, kama Yesu alivyofundisha.

Katika Ibada hii Papa aliiongoza akisaidiana na Kardinali Kurt Koch, Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Kukuza Umoja wa Kikristo na Katibu wake, Askofu Brian Farrell, na ili hudhuriwa na wajumbe na wafanyakazi wa Baraza hilo.

Papa alielekeza homilia yake zaidi katika somo la kwanza, ambamo mna maelezo jinsi Abrahimu alivyotolea maombi yake kwa Bwana kwa ujasiri na king'ang'anizi, ili ausalimishe mji wa Sodoma licha ya madhambi yaliyokuwa yakifanyika katika mji huo. Papa Fransisko alionyesha kuushangalia ujasiri huu wa Abrahim, kwa jinsi alivyopata nguvu za kuendelea kuzungumza uso kwa uso na Bwana, akiutetea mji huo wenye madhambi mengi, kama yanavyo sema Maandiko Matakatifu.

Papa alitafakati ujasiri huo, akianisha na wakati wetu, akisema,daima sisi tunapozungumzia ujasiri hufikiri juu ya ujasiri wa kitume, wa kwenda nje kuhubiri Injili na mambo kama hayo. Lakini kumbe, pia kuna aina nyingine ya ujasiri, ni ujasiri katika kutolea maombi mbele za Bwana. Ujasiri ambao mara nyingi, waamini hawana, wengi hukata tamaa haraka na kutokomea. Papa alieleza huku akionyesha mshangao kwa jinsi Ibrahimu anavyoshikilia ombi lake bila kuchoka hadi Bwana akamtimizia haja yake. Na ndivyo muumini anavyotakiwa kuomba kwa ujasiri na bila kuchoka , katika kuitetea haki hata ya mtu mmoja, ni kuomba wokovu hata kwa ajili ya mtu mmoja.
Papa aliendelea kusema kwamba, ni lazima kuomba kwa imani neema za Mungu na kumwacha yeye atende. Na alikumbusha kwamba, Yesu mwenyewe anatuambia kwamba lazima tuombe kama mjane au kama yule hakimu au kama yule mtu aliyekwenda kwa jirani yake katikati ya usiku na kubisha hodi mlangoni kuomba msaada kwa jirani yake, alibaki akigonga hadi jirani yake alipomtimizia haja yake.
Nasi waamini ndivyo tunavyotakiwa kuomba kwa imani, tukiendelea kunga'ngana hadi hapo Bwana atakapo timiza haja zetu kwa fadhila yake mwenyewe. Papa anasema ni vizuri kufanya hivyo. ,Maombi hayo ya Ibrahim, yanarejea katika moyo wa Yesu na kutufundisha, ombeni kwa ujasiri : maana Baba yeny anajua mnayo yahitaji.

Papa Fransisko alieleza na kuitazama zaidi zaburi ya 102: 'Mhimidini Bwana, Ee nafsi yangu; na yangu yote, lisifu jina lake Takatifu... na kusema kwamba, kwa naombi yaliyomo katika zaburi hii, tunajifunza mambo tunayopaswa kusema kwa Bwana wakati tunaomba neema.








All the contents on this site are copyrighted ©.