Kamwe msiboreke! Wamegeeni wengine furaha inayobubujika kutoka katika undani wa mioyo
yenu!
Jumapili iliyopita, tarehe 30 Juni 2013 Kanisa limeadhimisha Siku ya Ukarimu wa Khalifa
wa Mtakatifu Petro, ambayo waamini wanaalikwa kwa namna ya pekee kutoa michango yao
ya hali na mali kwa ajili ya kuchangia huduma ya upendo inayotolewa na Baba Mtakatifu
sehemu mbali mbali za dunia.
Papa Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji
wa mitandao ya kijamii, jumapili iliyopita, anawashukuru waamini wote kwa sala na
mshikamano!
Katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitando ya kijamii, anakumbusha
kwamba, kamwe Mkristo hapaswi "kuboreka" wala kuchukia. Anayempenda Kristo ni mtu
aliyesheheni furaha ambayo anawamegea wengine!