2013-06-27 08:05:55

Tume ya Kipapa kwa ajili ya Benki ya Vatican


Baba Mtakatifu Francisko ameunda Tume ya Kipapa kwa ajili ya Benki ya Vatican, (IOR) itakayofanya upembuzi yakinifu kuhusu masuala ya kisheria na shughuli mbali mbali zinazofanywa na Benki hii ili hatimaye, kufanya maboresho mintarafu maisha na utume wa Kanisa la kiulimwengu na Vatican katika ujumla wake. Tume hii inatekeleza katika mapana yake mabadiliko ambayo Baba Mtakatifu anapenda kufanya katika taasisi zinazoisaida Vatican kutekeleza utume wake.

Tume hii itakuwa na wajibu wa kukusanya taarifa kuhusu utendaji wa shughuli za Benki hii na taarifa yake kuwasilishwa kwa Baba Mtakatifu Francisko. Benki hii itaendelea kutekeleza wajibu wake mintarafu sheria ya mwaka 1990 iliyotolewa na Mwenyeheri Yohane Paulo wa pili au kama itakavyoamriwa vinginevyo na Baba Mtakatifu Francisko.

Tume ya Kipapa kwa ajili ya Benki ya Vatican inaundwa na Jopo la watu watano kama ifuatavyo:

Kardinali Raffaele Farina, Rais wa Tume.
Kardinali Jean Lous Tauran, Mwanachama.
Monsinyo Juan Ignacio Arrieta Ochoa de Chinchetru, Mratibu
Monsinyo Peter Bryan Wells, Mwanachama.
Professa Mary Ann Glendon, Mwanachama.







All the contents on this site are copyrighted ©.