Hali ya Mzee Nelson Mandela inaendelea kudhohofu zaidi na zaidi kiasi kwamba, kwa
sasa anapumua kwa kutumia mashine. Matumaini ya Mzee Madiba kuendelea kuishi yanazidi
kufifia kila dakika inayopita. Moja ya wanafamilia ya Mzee Madiba Napilisi Mandela
anasema, inasikitisha kumwona Mzee Madiba akiwa katika hali ile, lakini hawana loote
la kufanya kwa sasa, bali kuendelea kumwombea kwa Mwenyezi Mungu. Mzee Madiba, anapambana
na mauti kwa sasa!