2013-06-27 10:55:13

Maaskofu wasikitishwa na hukumu ya Mahakama kuu nchini Marekani!


Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani limesikitishwa na hukumu iliyotolewa na Mahakama kuu ya Marekani kuhusu sheria iliyokuwa inalinda ndoa ambayo ilianza kutumika kunako mwaka 1996 kuwa ni batili na kinyume cha Katiba. Tangu sasa watu wa jinsia moja wanaoishi kama mme na mke watakuwa na haki sawa kama watu wengine wanaoishi katika ndoa.

Katika taarifa iliyotiwa sahihi na Kardinali Timothy Dolan, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani anasema, kwamba, ndoa ni taasisi ya pekee inayomuunganisha mwanaume na mwanamke katika maisha na kwamba, watoto ni zawadi ya muungano huu wa upendo. Watoto wana haki ya kuwa na wazazi wa pande zote mbili yaani: Baba na Mama, changamoto kwa viongozi wa Jumuiya ya Kimataifa kulinda na kutetea maana hii ya ndoa.







All the contents on this site are copyrighted ©.