Sinodi za Maaskofu ni matunda ya Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican
Sekretarieti kuu ya Sinodi ya Maaskofu iliyoundwa kunako mwaka 2012 mara baada ya
Maadhimisho ya Sinodi ya Uinjilishaji Mpya iliyojadili kuhusu Uinjilishaji Mpya kama
nyenzo ya kutangaza Imani ya Kikristo, imehitimisha kikao chake cha nne, kilichofanyika
hapa mjini Vatican, chini uongozi wa Askofu mkuu Nikola Eterovic.
Katika utangulizi,
Askofu mkuu Eteovic amegusia kuhusu Maadhimisho ya Mwaka wa Imani ambao umeshuhudia
matukio makubwa ya kihistoria: kwanza ni lile la Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi
na sita, kwa hiyari na utashi kamili kuamua kung'atuka kutoka madarakani na badala
yake, Papa Francisko kuchaguliwa kuliongoza Kanisa Katoliki kama Khalifa wa Mtakatifu
Petro.
Wajumbe hao wamejadili kwa kina na mapana kuhusu Sinodi ya Maaskofu
wa Kanisa Katoliki kutoka Mashariki na Sheria zao; Mabaraza ya Maaskofu Katoliki,
Mabaraza ya Kipapa, Shirikisho la Wakuu wa Mashirika pamoja na taasisi ambazo zinashiriki
kwa karibu zaidi katika Maadhimisho ya Sinodi za Maaskofu.
Wajumbe wa Sekretarieti
pia walipata nafasi ya kukutana na kuzungumza na Baba Mtakatifu Francisko, aliyewachangamotisha
kuanza kutafakari kuhusu tema itakayofanyiwa kazi katika Maadhimisho ya Sinodi ya
Kumi na nne ya Maaskofu. Alikumbusha kwamba, Sinodi za Maaskofu ni matunda ya Maadhimisho
ya Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican, unaohimiza kwa namna ya pekee: umoja na mshikamano
miongoni mwa Maaskofu.
Huduma hii nimuhimu sana kwa Kanisa katika Mapambazuko
ya Millenia ya tatu ya Ukristo. Ni matumaini ya Baba Mtakatifu Francisko kwamba, Sinodi
zitaendelea kufanyiwa maboresho ili kukuza na kuimarisha mchakato wa majadiliano kati
ya Maaskofu na Khalifa wa Mtakatifu Petro.
Sekretarieti ya Sinodi imepata
nafasi ya kuweza kutafakari kwa kina tema, sababu na vigezo vilivyopelekea wajumbe
hao kuweza kuchagua, ili hatimaye, Baba Mtakatifu aweze kutoa uamuzi wa mwisho. Wajumbe
wa Sekretarieti ya Sinodi watakutana tena kuanzia tarehe 7 hadi 8 Oktoba, 2013