Tamasha la Muziki katika Maadhimisho ya Mwaka wa Imani
Baraza la Kipapa la uhamasishaji wa Uinjilshaji mpya linaloongozwa na Askofu mkuu
Rino Fisichella, mwishoni mwa Juma, liliandaa tamasha la muziki kwa ajili ya Maadhimisho
ya Mwaka wa Imani, lililofanyika mjini Vatican. Katika salam na matashi mema kutoka
kwa Baba Mtakatifu Francisko, alionesha pia kusikitishwa kwake kwa kutoweza kushiriki
katika tamasha hili kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wake.
Baba Mtakatifu
katika ujumbe wake uliosomwa kwa niaba yake na Askofu mkuu Rino Fisichella, aliwashukuru
wadau mbali mbali waliowezesha kufanikisha tamasha la Muziki kama sehemu ya Maadhimisho
ya Mwaka wa Imani. Ni tukio ambalo limewapatia fursa ya kusimama kidogo na kuinua
mioyo yao ya furaha na tafakari ya kina. Askofu mkuu Fisichella anasema, muziki ni
furaha na kiungo kwa watu mbali mbali.