2013-06-22 14:23:08

Mtanzania ashika hatamu za kuliongoza Baraza la FAO..


Shirika la Chakula na Kilimo FAO, Ijumaa katika Kikao chake lilimchangua Balozi Wilfred Joseph Ngirwa, kuwa Mwenyekiti mpya wa Baraza la FAO, kwa kipindi cha miaka miwili ijayo June 2013 hadi June 2015.

Balozi Wilfred Ngirwa, amechaguliwa kushika nafasi hii ya Mwenyekiti wa kujitegemea wa Baraza katika maana ya Mwenyekiti aliye huru asiyegemea upande wowote, kwa shindi wa asilimia 96 kati ya kura zote zilizopigwa na wajumbe wa Baraza 154, kura za ndio zikiwa 146, kura turufu 7 na kura za hapana 1( moja) .

Balozi Wilfred Ngirwa alizaliwa Tanzania mwaka 1948 katika familia ya kawaida ya Watanzania,Bukoba Mkoani Kagera. Ni mtalaam katika uwanja wa Kilimo na uchumi, kazi aliyoifanya wa muda wa miaka 38 , ambamo huduma yake ilitambulwia vyema hasa kwa mchango wake kama Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Tanzania na katika Mashirika matatu ya Umoja wa Mataifa yanayohusika na huduma kwa Mkulima, ambayo ni Shirika la Chakula na Kilimo(FAO) Shirika la Mfuko wa Maendeleo katika Kilimo( IFAD), na Shirika la Mpango wa Chakula (WFP). Na pia kama Mwakilishi wa Tanzania katika mashirika hayo,uwakilishi uliompa heshima ya kuwa Balozi.

Katika Khafla ya kumpongeza Balozi Ngirwa, iliyoandaliwa na Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Italy, Waziri wa Kilimo Tanzania, Mheshimiwa Waziri Christpher Kizza , alisema, ushindi wa Balozi Ngirwa katika kinyanyang’iro cha cheo hicho, umekuwa ni ushindi na heshima kubwa kwa Afrika, na hususani kwa Watanzania wote. Na hivyo ushindi huu ni changamoto inayodai hasa tanzania kwa ujumla kuendelea kuishi kwa amani na utulivu, katika kudumisha heshima ya Tanzania kwenye ngazi za Kimataifa, na kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania, na hasa Wakulima na wafugaji vijijini.

Waziri aliomba ushirikiano wa karibu na Mwenyekiti Mpya wa Baraza la FAO,akisema, ingawa kwa cheo chake hakifungamani na upande wowote, bado Afrika inatazamia kunufaika zaidi na mchango wake, katika kubadili maisha ya mkulima wa Afrika hasa kwa kutokana na uzoefu wake katika maisha yake ya kawaida ya mkulima wa Afrika Vijijini.

Na Balozi James Nsekela , katika hotuba yake fupi kwa Khafla hiii, alionyesha furaha yake kwamba Kupitia Balozi Ngirwa , Tanzania imeaminiwa kuliongoza Shirika la FAO. Aliiaja kazi hii kuwa ni nzito na nyeti yenye kuhitaji weledi na ushirikiano wa karibu na watendaji wengine. Vivyo katika Khafla hii alikuwepo Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Zanzibar, Dr gharib .

Na Balozi Ngirwa, alitoa shukurani zake za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Tanzania, Rais Jakaya Kikwete, kwa kuidhinisha jina lake liwakilishwe FAO, kama mgombea wa cheo cha Mwenyekiti wa kujitegemea katika Baraza la FAO. Na pia aliwashukuru wote, waliomtia moyo wa kugombea kiti hicho. Na kwamba akiwa katika cheo hiki kipya atafanya kazi zake katika misingi ya imani yake kwamba , FAO ni shirika ambamo misingi ya maamuzi yake imesimikwa katika misingi ya makubaliano ya nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa. Na hivyo, mamlaka yake yatazingatia rejea msingi zilizotajwa katika nyaraka za FAO, na Mpango wa Kidharura wa Utendaji kama ilivyo ainishwa katika hati za makubaliano za Fao.

Balozi Ngirwa anaanza Kazi yake Mpya Jumatatu 24 June 2013, katika makao makuu ya FAO , Mjini Roma.


Alhamis iliyopita, Papa Fransisko alikutana na wajumbe wa mkutano wa 38 wa FAO, ambamo katika hotuba yake Papa alikitaja kipeo cha njaa duniani kuwa ni kashfa kwa nyakai hizi ambamo mataifa yanajiita kuendelea na kustaraabika.

Na kwamba, kipeo hiki cha njaa dunaini hakiwezi kufutika hadi hapo hali ya mazingira na maisha ya watu hasa vijijini , kuchunguzwa katika mtazamo wa utu wa mtu na heshima yake kiutu.

Na alikumbusha kwamba, wote wanajua moja ya jambo linalotendea vibaya maisha ya mamillioni ya watu duniani na hasa vijijini ni ukosefu wa chakula, si tu kutokana na maafa asilia au migogoro na vurugu za kisiasa zinazopokonya watu mlo wao wa kila siku, lakini pia ukosefu wa uwajibikaji kwa walio nacho kutoa kwa wasiokuwa nacho ambao kwa wakati huu hutoa kama mabaki kutoka meza ya chakula. Alisisitiza wanapaswa kuchota toka ghalani kile kinachotakiwa kumfikia muhitaji mwingine kwa moyo wa upendo wa kweli..

Papa ameonyesha imani yake kwamba , kwa uzoefu wa wajumbe wa Mkutano huo unaofanyika kwa lengo la kushirikishana uzoefu na ufahamu utaweza kutoa mawazo ya kufaaa zaidi, kwa ajili ya kusisimiua utendaji wa kimataifa kwa niaba watu maskini wahitaji vijijini , wakiwa wamevuviwa si tu moyo wa hisani, ila upendo wa kweli katika kufuta kipeo hiki cha njaa duniani.









All the contents on this site are copyrighted ©.