2013-06-20 11:50:16

Zaidi ya wakimbizi 20,000 wamekufa maji wakijaribu kuvuka Bahari ya Mediterania!


Jumuiya ya Kimataifa inaadhimisha Siku ya Wakimbizi Duniani wakati ambapo kuna maelfu ya watu wanaendelea kupoteza maisha yao. Inakadiriwa kwamba, zaidi ya watu 20,000 wamefariki dunia wakijaribu kuvuka Bahari ya Mediterania, wakitafuta usalama na ubora wa maisha Barani Ulaya.

Wakimbizi wanaoishi nchini Italia wanakabiliwa na hali ngumu ya maisha, hasa wale wanaotoka katika maeneo ya vita na kinzani kama vile Syria, Lebanon, Yordan, Afrika ya Kaskazini, Somalia na Eritrea. Idadi ya wakimbizi wanaoomba hifadhi ya kisiasa inazidi kuongezeka mwaka hadi mwaka, lakini hali bado ni mbaya hasa katika kambi za wakimbizi. Haya yameelezwa na Mfuko wa kuhudumia Wakimbizi wa Baraza la Maaskofu Katoliki Italia, Migrantes.







All the contents on this site are copyrighted ©.