Umoja wa Mataifa walaani shambulizi lililofanywa na Kikundi cha Al Shabaab mjini Mogadisho
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki-Moon amelaani vikali shambulio lilofanywa
na kikundi cha Waaasi cha Al Shabaab kwenye Makao ya Shirika la Maendeleo la Umoja
wa Mataifa mjini Mogadisho, Somalia, Jumatano, tarehe 19 Juni 2013.
Katika
shambulizi hili watu kadhaa walipoteza maisha yao. Wachunguzi wa mambo wanasema kwamba,
Kikundi cha Shabaab bado kina nguvu ya kuendesha mashambulizi.