Watu wakimbia makazi yao kutokana na vurugu Sudan ya Kusini
Mapigano yaliyojitokeza hivi karibuni kati ya Jeshi la Serikali ya Sudan ya Kusini
pamoja na Kikundi cha Waasi katika eneo la Jonglei, yamepelekea idadi kubwa ya watu
kuyakimbia makazi yao kwa kuhofia usalama wa maisha yao. Shirika la Habari la Misna
linasema kwamba, kuna watu zaidi ya elfu kumi na moja wanaotafuta msaada wa dharura
kutoka Juba.
Wananchi hao wanalazimika kutembea kwa miguu umbali mrefu kabla
ya kupata msaada wa dharura unaotolewa na Mashirika ya Misaada ya Kimataifa Mjini
Juba.