2013-06-19 09:56:04

Viongozi wa Makanisa wapewa mafunzo ili kusimamia vyema mchakato wa uchaguzi mkuu nchini Zimbabwe!


Zaidi ya viongozi 200 wa kidini nchini Zimbabwe wamepewa mafunzo maalum yatakayowasaidia kufuatilia kwa ukaribu zaidi mchakato wa uchaguzi mkuu nchini Zimbabwe unaotarajiwa kufanyika mwaka huu. Mafunzo haya yalitolewa na Taasisi ya Kiekumene ijulikanayo kama "Christian Action Trust Zimbabwe" (CAT-Zim). Taasisi hii ina mpango wa kutoa mafunzo kwa viongozi wa Kanisa wapatao 5,000, ili kuhakikisha kwamba, mchakato wa uchaguzi mkuu nchini Zimbabwe unakuwa huru na wa wazi.

Kwa miaka kadhaa, Zimbabwe imekuwa ikishuhudia machafuko na madhulumu ya kisiasa yaliyopelekea taabu na mateso ya wananchi wa Zimbabwe ambao bado wanaendelea kulipia kasoro hizi. CAT-Zim ni mwanachama wa Baraza la Makanisa Ulimwenguni. Tarehe ya uchaguzi bado inaendelea kusababisha malumbano nchini Zimbabwe.







All the contents on this site are copyrighted ©.