2013-06-19 07:57:07

ONU inasikitishwa na idadi kubwa ya watoto nchini Mali kuwekwa kizuizini!


Umoja wa Mataifa umeonesha wasi wasi wake kutokana na ongezeko la watoto nchini Mali kuwekwa kizuizini kwa kizingizio kwamba wanashirikiana na Kikundi cha Waasi kinachoendesha shughuli zake Kaskazini mwa Mali. Akizungumza kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Bi Leila Zerrougui, Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa katika maeneo yenye kinzani na vita, anasema kwamba, katika siku za hivi karibuni kumekuwepo na ongezeko la watoto wanaoteseka kutokana na kuwekwa kizuizini.

Umoja wa Mataifa unataka haki msingi za watoto hao ziheshimiwe kadiri ya sheria na kanuni za kimataifa, jambo ambalo linapaswa kutekelezwa na Serikali ya Mali. Kuna dalili nyingi kwamba, nchini Mali haki za watoto zinaendelea kuvunjwa kwa kuwafundisha watoto ili kujiunga na vikosi vya kijeshi ili hatimaye, kupelekwa mstari wa mbele kwenye mapambano.







All the contents on this site are copyrighted ©.