Mkristo yuko tayari kujimwaga kutangaza Injili ya Kristo!
Wakati huu Mama Kanisa anapoendelea kuadhimisha Mwaka wa Imani, anawachangamotisha
watoto wake kujikita zaidi na zaidi katika Uinjilishaji Mpya. Baba Mtakatifu Francisko
anawaambia watumiaji wa mitandao ya kijamii kwamba, Mkristo daima yuko tayari kutangaza
Injili, kwani hawezi kuficha ndani mwake ile furaha ya kumtambua Kristo.