2013-06-19 16:25:41

Kwa fumbo la ubatizo sote tunakuwa viungo vya mwili mmoja wa Kristu, kanisa lake...Papa .


Katekesi ya Baba Mtakatifu Fransisko kwa mahujaji na wageni, imeelendelea kuitafakari sala ya Imani , na leo akitazamisha zaidi katika Kanisa kama Mwili wa Kristu.
alisema, Ndugu zangu wapendwa: Katika katekesi yetu juu ya sala ya Imani, leo tunaona Kanisa kama mwili wa Kristo. Kwa njia ya zawadi ya Roho Mtakatifu, tuliye mpokea katika Ubatizo, kimuujiza tunaunganishwa na Bwana kama kiungo cha mwili mmoja ambao Yeye ndiye ni kichwa. Na kwamba mfano wa mwili wa fumbo hili hutuwezesha sisi kuutambua umuhimu wa kuimarisha umoja wetu na Kristo kwa njia ya maombi ya kila siku,kusoma neno la Mungu, na kupokea sakramenti.
Papa Fransisko alieleza na kurejea waraka wa Mtume Paulo kwa Wakorintho, ambamo amesema kwamba, Mwili wa Kristo, ni mmoja ulioumbwa kwa viungo vingi. Na Ndani ya usharika wa Kanisa, na katika muungano na Papa na Maaskofu, kila mmoja wetu ana sehemu ya kutenda, na zawadi ya kushirikishana , huduma ya kutoa, katika kuujenga Mwili wa Kristo kwa upendo.
Papa aliwahimiza waamini kumwombe Bwana, ili atusaidie sisi kukataa kila aina ya utengano na migogoro tangu katika familia zetu, parokia na Makanisa. Na wakati huo huo, tuombe neema kufungua mioyo yetu kwa wengine, ili kukuza umoja na kuishi kwa amani na mapatano kama viungo vya Mwili mmoja wa Kristo, tukivuviwa na zawadi ya upendo unao miminwa na Roho Mtakatifu, ndani ya mioyo yetu.

Baada ya katekesi Papa alisamu katika lugha mbalimbali kulingana na lugh, pia akitaja makundi mbalimbali ya kijamii, vijana, wazee wanadoa wapya na bila kuwasahau wagonjwa. Kwao wote aliwapa baraka zake za Kipapa.

Na Mapema asubuhi, Papa Fransisko katika homilia yake alisema, Ukristo si kujifunza sheria na mausia tu , kwa kuwa kufanya hivyo kunaweza kuia kuelewa na kuuishi ukweli kwamba Mungu ni Mungu wa furaha na ukarimu. Papa alieleza wakati wa Ibada ya Misa mapema Jumatano hii katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta ndani ya Vatican..
Aliyarejea masomo ya siku akisema, wanafiki waandishi na mafarisayo, waliwabebesha watu wa Mungu mizigo ya sheria wasizoweza kuzibeba wao wenyewe na hivyo kuwaelekeza watu katika njia ya kifo.
Papa alieleza kwa kutafakari tabia tofauti tofauti kati ya waandishi na Mafarisayo, kama ilivyoandikwa katika Injili ya Mtakatifu Matayo ambamo mna wale wanaopenda kujionyesha wakati wa kusali, kufunga na kutoa sadaka. Lakini Yesu anawaambia wanafunzi wake mtoapo sadaka, sala na kufunga ni lazima iwe ni siri ili Baba anayeona sirini apate kuwapa ujira wenu.
Papa aliukosoa unafiki wa mafarisayo akisema si tu yalikuwa majivuno ya Mafarisayo na wanasheria , lakini pia hata leo kuna wenye kupenda kushinikiza sheria nyinginyingi ngumu kwa aamini.
Aliwaita watuwa namna hiyo kuwa ni manafiki , wasomi wasiokuwa na busara za kumtafuta Mungu , na kumwelezea Mungu katika muono mpana , na hivyo wanajizuia wao wenyewe na wengine pia kuuingia Ufalme wa Mungu.

Papa alifafanua, kumbe Bwana anazungumzia kufunga, maombi na Zaka, kuwa mihimili mikuu mitatu ya uchaji wa Kikristo, kwa ajili ya uongofu wa ndani, ambayo hupendekezwa na Kanisa kwetu sote hasa wakati wa kipindi cha Kwaresima. Pia alionya hata katika njia hii, kuna wanafiki, wanaopenda kujionyesha kwa kufunga, kutoa sadaka na kuomba. Papa ameasa , unafiki unapoingia katika hatua hii ya mahusiano na Mungu , inakuwa ni kutenda dhambi dhidi ya Roho Mtakatifu.








All the contents on this site are copyrighted ©.