2013-06-18 15:07:26

Waluteri na Wakatoliki- kuadhimisha pamoja siku ya Mageuzi


Kutoka Migogoro hadi Ushirika, ndivyo inavyoitwa hati ya pamoja ya Walutheri na Wakatoliki, inayo elezea safari yao ya kiekumeni ya miaka 50 iliyopita, wakati wakitazama mbele katika maadhimisho ya pamoja ya kutimia kwa miaka mia tano (500) ya Mageuzi katika Kanisa hapo mwaka 2017.

Jumatatu, Hati ya pamoja ya Tume ya Kimataifa ya Walutheri-Wakatoliki juu Umoja, iliwasilishwa katika mkutano wa waandishi wa habari, katika makao makuu ya Kilutheri, mjini Geneva. Hati inatazama kwa kirefu zaidi, sababu msingi za migawanyiko iliyotenganisha makanisa haya katika karne ya 16. Hivyo Tume , inashughulikia changamoto za uponyaji kumbukumbu hizo na kufanya kazi pamoja kwa ajili ya upatanisho na utoaji wa shuhuda kwa maoja duniani.

Mada zilizochunguzwa katika hati ni pamoja na msingi mandhari ya teolojia ya Martin Luther kwa lengo la mazungumzo kati ya Waluteri na Waktoliki, na pia inalenga katika kanuni tano za uekumeni , na kwa ajili ya mahusiano kati ya Makanisa yote, wakati wa adhimisho la pamoja kwa 2017.

Tarehe 31 Oktoba 1517, mtawa wa Ujerumani na msomi na mwana teolojia, Martin Luther, alitundika hoja zake 95, katika mlango Kanisa la Castle Wittenberg, alizoona zina haja ya kufanyika kwa haraka mageuzi. Mageuzi yaliyosababisha si tu utengano kati ya Makanisa ya Kiprotestanti na Wakatoliki, lakini pia kwa kiasi kikubwa kutoa changamoto nzito juu ya nafasi ya dini katika jamii.

Jumatatu , Mons. Mathiya Turk , Mkuu wa Mahusiano kati ya kanisa Kiluteri na Kipapa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Kukuza Umoja wa Kikristo, akiwa ameongozana na Rais wa Baraza hilo la Kipapa, Kardinali Kurt Koch, mjiini Geneva, waliwasilisha hati kwa pamoja katika wa vyombo vya habari.
Mathiya Turk, akizungumza na Phillipa Hitchen, juu ya umuhimu wa hati hiyo ya pamoja , aliitaja kuwa ni muhimu sana kihistoria baada ya karne nyingi za migogoro na kutoelewana, na kusababisha hata vita kati ya mataifa na ndani ya nchi. Na Maadhimisho yajayo yatakuwa ni ya kwanza kufanyika pamoja kiekumene. Alieleza na kulezea tamko lililokwisha tolewa na Martin Junge, ambaye ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Kilutheri Duniani, kwamba maadhimisho haya yatakuwa ya kimataifa, hivyo ni vyema, kuwa ya kiekumene na ni wito kwa waamini wa makanisa kushuhudia kimatendo umoja ulioombwa na Kristu mwenyewe.

Na kwamba , sababu ya mgawanyiko wa Kanisa, mara nyingi tafasiri hukosewa na hivyo kwa mtazamo huo hata tafasiri zake katika imani, teolojia na kidini. Kwa hiyo, katika mazungumzo ya kimataifa ya kiekumeni, wamekuwa na uwezo wa kugundua upya misingi ya kawaida katika maswali haya ya imani na waweza, kuwa na uwezo wa kueleza kwamba, hizi si sababu tena za kuligawa Kanisa. ....

Na kwa upande wa Wakatoliki, imani juu ya mabadiliko ndani ya Kanisa, yanakubalika kama ni ni jambo la kawaida katika safari yake 'Ecclesia Semper reformanda' – ni kwamba maisha ya kanisa daima ni kutembea na marekebisho wakati wote na katika kila umri, hivyo jambo la mageuzi linakuwa la kawaida pande zote mbili, nini wameweza kufanya katika hati hii, ni kuonyesha mada kuu ya teolojia ya Martin Luther kuwa yamekuwa ni maswala kwa ajii ya kanisa zima na vipengere muhimu vya mageuzi katika Kanisa.








All the contents on this site are copyrighted ©.