Papa awaambia Waroma; Ninyi ni Mashahidi jasiri na wagonjwa
Jumatatu jioni, ukumbi wa Paulo V1 wa mjini Vatican, ulijaa nyuso za furaha na kicheko
za mamia ya waamini kwa ajili ya Mkutano wa Kikanisa wa Jimbo la Roma uliofanyika
chini ya Mada Kuu: Kristo muhimu: Jukumu la Wabatizwa kumtagaza Yesu Kristo. Katika
kufungua kazi za Mkutano huu, Papa Francisko, kabla ya kuingia ukumbini , pia alisalimia
mamia ya waamini, waliobaki nje kufuatilia tukio hili nje kupitia Skrini kubwa ya
Televisheni. Ilani ya Katekesi ya Papa kwa ajili ya tukio hili , iliongozwa na
Kauri mbiu:, Mimi sina aibu kuitangaza Injili, na alieleza juu ya dhamira ya sasa
katika Uinjlishaji jimboni Roma na makandokando ambamo sasa kuna mabadiliko makubwa
jamii ya kumezwa na hali za kidunia. Katika mkutano huu akiwepo pia Kardinali Agostino
Vallini, Vika Mpya wa Jimbo la Roma. Katekesi ya Papa, illiyojaa maisha sala,
na tafakari zilizo lenga Ubatizo, Uinjilishaji na ujirani mwema kwa wakazi wa Roma,
hasa maskini na watoto wadogo. Mimi siionei aibu Injili ...Na kwenu wabatizwa
hamko chini ya sheria bali chini ya neema. Papa ulitoa maneno haya ya Mtakatifu Paulo
kwa Warumi, kama kielelelzo dhahiri katika katekesi yake, kueleza nini maana ya kuishi
chini ya neema na uhusiano wake na uinjilishaliji. Neema ni furaha yetu, ni uhuru
wetu kama wana wa Mungu ni mageuzi yaliyo badilisha moyo wa dhambi na katika utakatifu
, kama Mtakatifu Paulo . Hii neema tuliyopewa bure lazima kuitoa, kwa moyo wa ukarimu
na shukurani na uhuru kamili kwa wengine. . Hivyo ni rejea inaoelekeza katika hali
halisi za raia wa Roma na wale wanaotafuta matumaini la kweli katika jamii na hawawezi
kuipata huko.
Papa alieleza na kurejea hali zingine nyuma na za kuumiza zinazokabili
wakazi wa Jimbo la Roma, ambamo alisema kuna wengi waliopoteza imani na wasiokuwa
na matumaini. Hivyo alimtaka kila aliyekuwa akimsikiliza kufikiri kwa makini, na katika
hali ya ukimya wa ndani ,juu ya watu hawa ambao wanaishi bila tumaini, wakiwa wamemezwa
na huzuni kubwa na masononeko mengi ndani , wanaotoka kuzitoka hali hizo lakini wanatumia
njia zisizoweza kuwatoa katika mahangaiko hayo, kama ulevi wa kupindukia katika unywaji
wa pombe, dawa ya kulevya, kucheza kamari, fedha na ngono za fujo, mambo yasiyoweza
kuwatoa katika shida zao.
Papa aliwahimiza waamini kwamba, ni i lazima kulionyesha
tumaini na furaha ya Mkristu kwa watu hao. Lakini kwa namna gani? Ni rahisi, Papa
alieleza, ni kupitia tabasamu na shuhuda msingi za ushindi wa Mkristu dhidi ya mambo
ya kidunia. Lakini ushuhuda huu unahitaji ujasiri na uvumilivu, tabia mbili za Mtakatifu
Paulo na Wakristo wote, na wale wanaotoka na kwenda kukutana na watu,waliotupwa pembezoni
na hali za maisha. Papa alikamilisha na kuialika jamii, kujenga ujasiri na uvumilivu,
kwao wenyewe kwanza, ndipo watoke nje na kwenda huko ambako wanaume na wanawake wanaishi
, kufanya kazi na kuteseka katka kuitangaza huruma ya Mungu, inayowafanya watu kumtambua
Yesu Kristu wa Nazareti. Kutangaza Neema hii, tuliyopewa na Yesu .
Papa alieleza
na kutahadharisha uwepo wa adui wengine, wanao wafanya waamini kuwa dhaifu katika
uinjilishaji , akitaja kukata tamaa na woga, vinavyo shamirishwa na shetani ndani
yetu: na hivyo kutengeneza vita vya kiroho, vyenye kuua Wakristu wengi, ambavyo
ni lazima kuwa tayari, kupambana. Hakuna sababu za kuogopa kwa sababi silaha
katika mapambano haya ni upendo, upendo wa Mungu, Baba yetu. Usiogope kupokea neema
ya Yesu Kristo, wala kuwa na hofu juu ya uhuru wako, kwa kuwa uhuru huo unatoka katika
neema ya Yesu Kristo, au, kama Paulo alisema, "wewe si chini ya Sheria bali chini
ya neema. Papa alihoji wake kwa waume waliokwisha ipokea neema hiyo wakati wa Ubatizo,
inakuwaje wanaogopa kuitangaza? Ni neema ambayo Yesu anawapa waamini , neema isiyo
gharamu kitu, bali kuipokea na kuitunza.