Bwana Ken hackett ateuliwa kuwa Balozi wa Marekani mjini Vatican
Rais Barack Obama wa Marekani amemteua Bwana Ken Hackett, kuwa Balozi wa Marekani
mjini Vatican. Bwana Hackett kwa takribani miaka 40 amekuwa akifanya kazi na Shirika
la Misaada la Kanisa Katoliki nchini Marekani hadi mwaka 2012. Amewahi pia kufanya
kazi zake Afrika Mashariki, Sierra Leone na pia kama Balozi wa Marekani nchini Ufilippini
kuanzia mwaka 1987 hadi mwaka 1992.
Kuanzia mwaka 1996 hadi mwaka 2004 alikuwa
ni Makamu wa Rais Caritas Internationalis nchini Marekani. Kati ya mwaka 1996 hadi
mwaka 2011 alikuwa ni mjumbe wa Cor Unum. Na mwaka 2004 hadi mwaka 2009 alikuwa ni
Mkurugenzi wa bodi ya wakurugenzi wa MCC. Uteuzi huu unasubiri kuthibitishwa na Congress
ya Marekani.