Uchumi wa kimataifa, mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa; ulinzi na usalama
ni kati ya mambo makuu yanayojadiliwa na Wakuu wa G8 wanaoanza mkutano wao mkuu wa
mwaka kuanzia tarehe 17 hadi 18 Juni 2013 huko Ireland ya Kaskazini. Syria, Afghanstan
na Bara la Afrika ni kati ya masuala tete yanayojadiliwa na viongozi hawa pamoja na
Wawakilishi kutoka Barani Afrika.
Wakuu wa G8 wanajadili pia mbinu mkakati
utakaoziwezesha nchi zao kuvuka kikwazo cha athari za myumbo wa uchumi kimataifa ambao
umepelekea ukosefu wa ajira kwa vijana wengi duniani pamoja na kuendelea kufanya mabadiliko
makubwa katika Shirika la Fedha Kimataifa.