Mwezi Juni, Mama Kanisa anafanya Ibada kwa Moyo Mtakatifu wa Yesu kielelezo cha huruma
na upendo wa Kristo kwa waja wake. Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa
watumiaji wa mitandao ya kijamii anaombea ili daima Kanisa liwe ni mahali pa huruma
na upendo wa Mungu; mahali ambapo kila mtu anajisikia kupendwa na kusamehewa!