Mheshimiwa Padre Xavier Munyongani ateuliwa kuwa Askofu Mpya wa Jimbo Katoliki la
Gweru, Zimbabwe
Baba Mtakatifu Francisko amemteua Mheshimiwa Padre Xavier Munyongani wa Jimbo Katoliki
la Masvingo, Padre mshauri wa maisha ya kiroho wa Jumuiya ya Waamini wa Kanisa Katoliki
kutoka Zimbabwe wanaoishi nchini Uingereza kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki la Gweru,
nchini Zimbabwe.
Askofu mteule alizaliwa tarehe Mosi, Januari 1950 Jimboni
Masvingo. Baada ya masomo na majiundo yake ya Kikasisi, akapadrishwa kunako tarehe
20 Agosti 1977 kwa ajili ya Jimbo Katoliki Gweru na baadaye, akajikuta akiwa kwenye
Jimbo la Masvingo lililoundwa kunako mwaka 1999.
Jimbo Katoliki la Gweru lilianzishwa
kunako mwaka 1955 ni sehemu ya Jimbo kuu la Bulawayo, Zimbabwe. Jimbo lilikuwa wazi
kuanzia mwezi Aprili 2012 baada ya Askofu Martin Munyanyi kung'atuka kutoka madarakani.