Mtumishi wa Mungu Odoardo Focherini kutangazwa kuwa Mwenyeheri
Mama Kanisa tarehe 15 Juni 2013 anatarajia kumtangaza Mtumishi wa Mungu Odoardo Focherini
kuwa Mwenyeheri. Huyu ni mwamini mlei, baba wa watoto saba, mwandishi wa habari na
mkurugenzi wa Gazeti la “L’Avvenire di Italia” huko Capri, Kusini mwa Italia. Oduardo
Focherini aliuwawa kikatili kutokana na chuki za kiimani. 00:00:50:50
Ni
mwamini mlei aliyejitoa kimaso maso kwa ajili ya kuwalinda na kuwaokoa Wayahudi zaidi
ya 100 waliokuwa wako hatarini kupelekwa uhamishoni. Kitendo hiki kilihatarisha maisha
yake, kiasi kwamba, akakamatwa na kutiwa gerezani kutokana na chuki dhidi ya Imani
ya Kanisa Katoliki.
Kutokana na mateso na madhulumu makali, kunako mwaka 1944
akaitupa mkono dunia, akiwa kijana mwenye umri wa miaka 37. Ni mwamini wa kwanza kutoka
Italia kutangazwa na Mama Kanisa kwa kusimama kidete kulinda na kutetea maisha ya
Wayahudi dhidi ya dhuluma na nyanyaso za utawala wa Kinaz