Papa aonya hatari za kuwa na miungu wadogowadogo kisirisiri
Baba Mtakatifu Fransisko, amewaonya Wakristu kutotunza miungu wadogowadogo wa kisirisri
ambao huharibu maisha na mwenendo wao kwa Mungu mmoja. Onyo hilo alilitoa Alhamis,wakati
wa Ibada ya Misa mapema Asubuhi katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta. Alisema njia
pekee iendayo kwa Mungu, ni kumpenda Mungu kama Yesu alivyofundisha.
Kama
ilivyo desturi ya ikila siku kutoa tafakari ya masomo ya siku, ambamo somo la Injili
lilieleza juu ya Mwandishi aliyemwendea Yesu na kuuliza ni ipi amri ya kwanza katika
amri zote. Papa Fransisko alibainisha kwamba, pengine swali hili ni swali la hila
la kumjaribu Yesu kama kwali analo jibu sahihi.
Maneno ya mwandishi huyo,
yaliyonukuu Biblia, Sikiliza Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana peke yake! Na
Yesu akamjibu na maneno , Wewe huko mbali na Ufalme wa Mungu. Papa Franssisko anasema
kwamba, kwa maneno hayo, kwamba wewe si mbali na Ufalme wa Mungu, Yesu alitaka kumwambia
mwandishi huyo, wewe unajua nadharia vizuri sana, lakini wewe bado uko mbali kutoka
ufalme wa Mungu, maana kw amana kwamba, anahitaji kuongeza mwendo wa kubadilsiha
amri hizi katika hali halisi za maisha , kwa sababu tunamkiri Mungu kupitia njia yetu
ya maisha.
Haitoshi kusema lakini naamini katika Mungu, Mungu mmoja pekee.
Hilo ni sawa, lakini ni jinsi gani unaweza kuishi hivyo katika safari ya maisha yako?Kwa
sababu tunaweza kusema, 'Bwana ni Mungu mmoja tu, hakuna mwIngine,lakini hali halisi
ya maisha yetu hazishuhudii uwepo wa Mungu pekee. Yanaonyesha uwepo wa miungu wengine
katika makandokando yetu... Hii ni hatari, kwa kuwa miungu wengine hutuletea roho
wa kidunia, roho wa tamaa, roho wa uchoyo, chuki, ubinafsi n.k.
Papa alikumbusha
Yesu mwenyewe aliliweka wazi , hapana kwa Roho wa Kidunia katika sala yake ya wakati
wa karamu ya mwisho, Baba utuopoe na roho wa ulimwengu, kwa sababu roho ya ulimwengu
hutuongoza katika ibada za miungu wengine.
Papa Fransisko aliendelea: kuzungumzia
ibada katika miungu wengine akisema sote tuna miungu wa kisirikisiri waliofichika
lakini hujionyesha katika njia ya maisha ya tunayofuata. Na ili kuondokana na miungu
hao wenye kutuweka mbali na ufalme wa Mungu ni kuwagundua miungu hawa wa kisirisiri
waliofichika katika roho zetu.
Papa alieleza na kumrejea Rahel, mkewe Yakobo,
aliye jifanya hana miungu wengine na kumbe, ana sanamu aliyochukua kutoka nyumba
ya baba yake na kujificha katika matandiko yake. Papa alisema kwamba sisi pia "zimeficha
miungu wetu wa sirisiri katika matandiko yetu ... inabidi kuwatafuta na kuwaangamiza
kwa sababu njia pekee ya kumfuata Mungu ni njia ya upendo ambayo na msingi wa upendo
huo, ni uaminifu.
Na uaminifu hutudai kuwafukuza miungu wote wadowadogo nje
ya mioyo yetu, ambao huonekana katika tabia na mienendo yetu ya maisha. Mtume Yakobo
anasema,.. Anayetaka kuwa mpenzi wa malimwengu, huwa adui wa Mungu.