2013-06-07 11:30:46

Acheni mazoea ya kutupa chakula!


Baba Mtakatifu Francisko anawakumbusha watumiaji wa mitandao ya kijamii kwamba, ulaji wa kupindukia umewatumbukiza watu wengi katika mazoea ya uharibifu wa chakula. Lakini, ikumbukwe kwamba, chakula kinachotupwa ni sawa na kumwibia maskini na mwenye njaa!

Katika Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani kwa Mwaka 2013, Katibu mkuu wa umoja wa Mataifa bwana Ban Ki-Moon ameitaka Jumuiya ya Kimataifa kuweka mikakati thabiti itakayosaidia kudhibiti uharibifu wa chakula kama sehemu ya mbinu mkakati wa kupambana na baa la njaa duniani.

FAO inabainisha kwamba, tani billioni 1.3 za chakula hutupwa kila mwaka, wakati kuna mamillioni ya watu wanateseka na kufa kwa baa la njaa na utapimlo.







All the contents on this site are copyrighted ©.