2013-06-04 09:29:17

Ukosefu wa fursa za ajira bado ni tatizo sugu duniani kwa mwaka 2013


Shirika la Kazi Duniani limetoa taarifa ya hali ya fursa za kazi duniani kwa kuonesha kwamba, ukosefu wa fursa za ajira ni tatizo ambalo linazikumba nchi nyingi duniani. Kuna dalili za kukua na kuboreka kwa uchumi katika nchi nyingi, lakini hali bado ni tete sana. Dalili hizi zimejionesha katika nchi zinazoibukia katika uchumi kama vile Brazil, India na Afrika ya Kusini pamoja na baadhi ya Nchi zinazoendelea.

Lakini takwimu zinaonesha kwamba, katika nchi tajiri duniani kuna idadi kubwa ya watu wasiokuwa na fursa ya ajira, jambo ambalo linaendelea kukua na kuongezeka maradufu, ikilinganishwa na miaka kadhaa iliyopita. Tatizo hili linaendelea kuibua makundi ya watu ndani ya Jamii: maskini wa kutupwa na kundi dogo la matajiri.

Baadhi ya Makampuni yameaanza kupata faida baada ya miaka kadhaa ya athari za myumbo wa uchumi kimataifa. Uwekezaji bado uko katika kiwango cha chini sana, kiasi ambacho si rahisi kufufua uchumi kwa haraka kama wengi wanavyotarajia.







All the contents on this site are copyrighted ©.