2013-06-04 15:35:19

Papa Fransisko alaani ukani Mungu kwamba ni hatari kwa jumuiya ya Kikristu.


Papa Fransisko Jumatatu akiongoza Ibada ya Misa ya Asubuhi, katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta,homilia yake ililenga zaidi katika mambo matatu, dhambi, ukani Mungu na utakatifu. Papa alisema, ukani Mungu, hufanya madhara makubwa kwa Kanisa, kwa sababu mtu anayemkana Mungu, hujitukuza mwenyewe, kinyume na Watakatifu ambao hutenda mengi kwa ajili ya manufaa ya wengi na kanisa. Hivyo Watakatifu ni mwanga wa maisha adilifu ya Kanisa.

Papa alieleza hilo, kwa kurejea somo la Injili ambamo alitaja kile kinachotakiwa kufanywa, kwa ajili ya kuwa wamiliki wa shamba la Bwana la mizabibu. Alitaja makundiya matatu ya watu wanaoishi katika shamba la Bwana kuna wenye dhambi, wakani Mungu, na watumishi wa Mungu.
Papa alisema, hakuna haja ya kuzungumzia sana dhambi, kwa sababu sisi wote ni wadhambi. Na hili tunalitambua toka ndani ya mioyo yetu, na kama mtu hana hisia hizo kwamba ni mwenye dhambi, ajione kuwa amepungukiwa na atafute msaada wa daktari wa kiroho. Aliendelea kuuchambua mfano huo wa shamba la mizabibu, akimrejea mtu mwingine, anayetaka kumiliki shamba hilo la mizabibu lakini kwa kupoteza uhusiano wake na Bwana wa shamba, Mwalimu ambaye, ametuita kwa upendo, mwenye kutulinda na kutupatia uhuru kamili .

Papa alitahadharisha hatari ya uhuru huo, unapokuwa katika mwelekeo wa kutaka kujitegemea, kujitenga mbali na Mungu, na moyo wa kujiona umejikamilisha katika yote na hivyo kuona hakuna haja ya Mungu kungilia kati maisha.. Moyo wenye kuwa na mwelekeo huo , hujenga ufisadi. Na kwamba mafisadi hawa , walianza kuwa wadhambi kama sisi, Lna kuendeleea hadi kuongeza hatua nyingine zaidi ya inayo wathibitisha katika dhambi yao, kuona hawana haja ya Mungu, licha kwamba, kanuni asili ya maumbile ya binadamu katika uhusiano wake na Mungu, haufutiki. Na kwa kuwa hawawezi kukanusha hili, wakani Mungu, hujitegenezea miungu wa bandia, hivyo kuwa mafisadi wa imani.

Papa amewaasa kwamba, wakani Mungu hujifikiria wenyewe tu , kuwa ndiyo kundi zuri. Lakini katika ukweli wake, hujilinganisha wa maisha ya jamii ya Kikristo, ni watu walio jinasua wao wenyewe wamejinasua na kujiweka nje. Papa alieleza na kutolea mfano wa Yuda aliye msaliti Yesu, ambaye kwanza alitenda dhambi ya tamaa, na kupotelea katika ukani Mungu.
Papa anaonya barabara hii ya uhuru ni barabara ya hatari, ambamo wakani Mungu huwa wasahaulifu sana, husahau upendo wa Bwana uliowapa kuwa wamiliki wa shamba la Bwana , na kuharibu uhusiano wao na Bwana, na kujitenga na mahusiano na upendo huu, na kuwa na tabia ya kujiabudu wenyewe. Ukana Mungu huu ni hatari kubwa katika jamii ya Kikristo! Papa amemwomba Bwana awaokoe Wakristu wote wakati wanapotembea katika barabara hii ya imani ili wasitelezee chini katika barabara ya ukani Mungu.

Papa alikamilisha hotuba yake kwa kurejea maadhimisho ya miaka hamsini ya kifo cha Papa Yohane XXIII, "mfano wa utakatifu." Katika Injili ya leo, aliongeza, Watakatifu ni wale waliokwenda kukusanya kodi katika shamba la Bwana, wakijua Bwana wao anachokitarajia kutoka kwao, na wakafanya kila jitihadi ya kutimiza wajibu wao. Watakatifu ni wale wanao Mtii Bwana, watu wa ibada kwa Bwana, ni wale ambao bado hawajapoteza kumbukumbu ya upendo wa Bwana, aliyewaweka katika shamba lake la mizabibu, hawa ndiyo watakatifu katika Kanisa.
Kama ilivyo ukani Mungu huleta madhara mengi kwa Kanisa,ndivyo ilivyo kwa Watakatifu hufanya mambo mengi mazuri. Mtume Yohana anasema "Ukani Mungu ni adui wa Kristo, ingawa wao hutoka miongoni mwetu na kuishi kati yetu, lakini wao wanakuwa tena si wa kwetu."
Katika Ibada hiyo , Papa aliomba kwa Bwana, neema ya kuelewa kwamba sisi ni wenye dhambi, wadhambi wa kweli katika asili yake.. Lakini si wakani Mungu.Pia aliomba Neema ya kutembea katika njia ya utakatifu. Na iwe hivyo. "

Katika Ibada hii, Papa aliongoza Ibada akisaidiana na Kardinali Angelo Amato, Mkuu wa Shirika kwa ajili ya Maisha Matakatifu na ilihudhuriwa na kundi la Maaskofu, mapadre na kikundi cha maofisa kutoka jengo la Kipapa.








All the contents on this site are copyrighted ©.