Jifunzeni kutoka kwa Bikira Maria kutenda kwa ujasiri!
Baba Mtakatifu Francisko anawaambia watumiaji wa mitandao ya kijamii kwamba, wakati
mwingine wanafahamu kile wanachopaswa kutenda, lakini hawana ujasiri wa kulitenda
jambo hili. Anawaalika watumiaji wa mitandao kujifunza kutoka kwa Bikira Maria namna
ya kufanya uamuzi kwa kujiaminisha kwa Mwenyezi Mungu.