2013-06-03 09:18:46

Uchaguzi Zimbabwe unapaswa kufanyika katika kipindi cha miezi miwili kuanzia sasa!


Mahakama kuu ya Zimbabwe inaitaka Serikali kuhakikisha kwamba, inafanya uchaguzi mkuu nchini humo katika kipindi cha miezi miwili, kabla ya tarehe 29 Julai 2013 wakati ambapo Bunge la sasa litakuwa linakamilisha muda wake rasmi. Vyama mbali mbali vya kisiasa nchini Zimbabwe vinatakiwa kuanza kujipanga kikamilifu ili mchakato wa uchaguzi mkuu wa Rais na Wabunge uanze mara moja.

Itakumbukwa kwamba, Serikali iliyoko madarakani kwa sasa ni ile ya kitaifa, baada ya kutokea machafuko ya kisiasa nchini Zimbabwe kunako mwaka 2008, Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe na Bwana Morgan Tsvangirai wakalazimika kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Rais Mugabe anataka uchaguzi ufanyike mara moja!

Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa Zimbabwe Bwana Morgan Tsvangirai anapendelea kwanza kufanyike mageuzi makubwa katika sheria, vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na sheria za uchaguzi. Uchaguzi mkuu wa Zimbabwe unatarajiwa kufanyika chini ya Kabisa Mpya iliyopitishwa hivi karibuni kwa wananchi wa Zimbabwe kuipigia kura ya maoni, baada ya vuta nikuvute ya vyama vya kisiasa nchini Zimbabwe.







All the contents on this site are copyrighted ©.