2013-06-03 15:47:20

Papa aongoza Ibada ya kuabudu Ekaristi Takatifu.


Jumapili 2 June, mamilioni ya wakatoliki duniani kote walijumuika katika makanisa wakitolea muda wao katika saa ya Kuabudu Ekaristi Takatifu, kama alivyoomba Papa Fransisko, dunia ya waamini wote wka pamoja majira ya saa kumi na moja na nusu za jioni, wawe mbele ya Kristu aliye hai ndani ya Ekaristi Takatifu.
Papa Fransisko , aliliongoza tukio la hili, bila ya kutazamiwa, katika Kanisa Kuu Mtakatifu Petro la Vatican. Watu waliweza pia kufuatilia tukio hili, katika njia za mawasiliano jamii, televisheni, redio na mtandao wa internet.
Baba Mtakatifu aliomba wakati huu wa Kuabudu Ekaristi, maombi yatolewe ili kwamba, Kanisa liweze kuenea duniani kote , na katika mjumuiya wa waamini kwa wakati mmoja , saa ya ibada kwa Ekaristi Takatifu, iwe ishara ya umoja wa Wakristu. Papa alisali ili kwamba Bwana, awezeshe Kanisa kuwa tiifu zaidi katika kusikia Neno la Bwana, na ili uziri wake uweze kung'ara mbele dunia kwa watu wote kuona manufaa yake, bila ya kupakazwa na matope ya dhambi na kashfa, lakini likiwa takatifu na bila lawama zisizokuwa na misingi. Pia Ili kwamba, kupitia tangazo lake aminifu,juu ya Neno linalo okoa wengi, liendelee kutoa mwangi wa huruma ya Mungu na kuongeza upendo katika kupata maana kamili ya maumivu na mateso, kwamba ni furaha na utulivu.
Na ili kwamba, kwa wale wote ambao hata leo hii, wapo katika pande mbalimbali za dunia, ambao bado wanakabiliwa na mateso ya hali , au kuathiriwa na vita, biashara ya binadamu, soko la madawa ya kulevya, na sulubu ya kazi ngumu za kitumwa, waweze kuuona mwanga wa kuokoka katika mateso hayo. Papa pia alitolea sala kwa ajili ya watoto na wanawake wanaokabiliwa na maisha magumu na hatarishi kutokana na kila aina ya vurugu na madhulumu.
Pia aliomba ili kwamba, ukelele wa kimyakimya unaotafuta msaada, uweze kusikika na kusikilizwa na Kanisa hai, linalo mkazia sana macho Kristu Msulubiwa, lisiweze kuwasahau ndugu hawa wake kwa waume, walio sahaulika na kuachwa katika huruma ya vurugu. Pia, kwa wale wanaojikuta katika hali halisi ngumu za kiuchumi, hasa katika kupambana na ukosefu wa ajira, wazee, wahamiaji, wasio na makazi, wafungwa, na wale wote wanaobaguliwa na kunyanyasika katika jamii kutokana na hali zao duni. Ili kwamba sala ya Kanisa na juhudi zake za kuwafariji na kuwapa msaada katika tumaini, zipate nguvu na ujasiri katika kutetea hadhi ya kila binadamu.

Ibada ya kuabudu Ekaristi Takatifu , iliongozwa na somo la Injili ya Yohane sura ya sita, ambamo Yesu anazungumzia Ekaristi. Ibada hiyo pia ilipambwa kwa nyimbo za kijadi juu ya Ekaristi. Na pia kulitolewa maombi ya Mapapa sita tangu wa Papa Pius XII hadi Papa Benedict XVI, wakati huo wa kuabudu, na pia kwa ajili ya mahitaji mengine ya wanadamu wote.

sherehe alihitimisha kwa Wimbo wa "Tantum Ergo" na Baraka Takatifu za Ekaristi iliyobarikiwa na Papa Francis.








All the contents on this site are copyrighted ©.