2013-06-03 15:58:53

Ongokeeni Imani kwa Matumaini


Jumapili, Baba Mtakatifu Fransisko, akiuhutubia umati wa waamini mahujaji na wageni zaidi ya laki moja, waliokusanyika katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, nyakati za Sala ya Malaika wa Bwana, aliwaaambia, Siku Kuu ya Mwili na Damu ya Kristu , inatuita katika wogofu wa matumaini, kuweza kugawa kidogo tulicho nacho na kamwe tusibaki tumejifungia wenyewe ndani kwa woga wa kuishiwa..

Papa alitoa hotuba yake akiirejea Siku Kuu ya Alhamis, ambayo ilikuwa ni Maadhmisho ya Mwili na Damu ya Kristu ( Corpus Christi), ambayo nchini Italia na pia katika mataifa mengine mengi, iliadhimishwa rasmi siku ya Jumapili.
Papa Katika hotuba yake alirejea somo ya Injili, juu ya muujiza wa mikate (Luka 9:11-17), akilenga zaidi katika hali ilivyokuwa siku hiyo katika pwani ya Ziwa Galilaya, ambako jioni inajongea na watu wengi bado wamekusanyika kwa Yesu kw amuda wa saa nyingi na hivyo wana njaa. Na wanafuzi wa Yesu wajadiliana juu ya tatizo la watu hao watakula nini, na hivyo kumuomba Yesu, atawanye watu ,ili kila mmoja atafute mbinu zake za kujipatia chakula. Lakini Yesu anawajibu, Wapeni ninyi chakula (mstari 13). wanafunzi ni kwa haraka nao wakajibu tuna mikate mitano na samaki wawili, wa kuwatosha wao.

Papa Fransisko alisema, Yesu alijua vizuri sana nini cha kufanya, lakini alitaka kuwahusisha wanafunzi wake, alitaka kuwafundisha, kwamba Mtazamo wao wanafunzi ni wa kibinadamu, unaotafuta ufumbuzi wa tatizo katika hali halisi na jawabu la kibinadamu lisilotaka kuzua matatizo mengine. Waache watu waende zao, ili kila mmoja ajipangie atakula nini. Na pia wanafunzi walimhurumia Yesu wakitaka apate muda wa kupumzika., kwa kuwa alikuwa tayari kafanya mengi kwa ajili yao , kuwahubiri na kuwaponya wagonjwa. Na sasa basi waache waende zao.

Mtazamo wa Yesu, kwa wanafunzi wake, unakuwa tofauti kabisa. Yesu anaonyesha kuwa na muungano na Baba yake wa huruma kwa watu. Yesu mwenye huruma, anayajua matatizo yao, mapungufu yao, na mahitaji ya watu, na ndivyo ilivyo hata kwetu sisi sote.
Yesu aliiona hiyo mikate mitano , kuwa tayari ni riziki , kwamba kutoka vitu hivi vichache, Mungu anaweza kuzalisha kile ambacho ni muhimu kwa kila mtu. Yesu anaiweka imani yake kamili kwa Baba wa Mbinguni kwa utambuzi thabiti kwamba kwa Yeye kila jambo linawezekana . Na hivyo anawaagiza wanafunzi wake , kuwaketisha watu katika makundi ya watu hamisini hamsini.
Papa anafafanua , watu kuketishwa katika makundi makundi ya watu hamisni hamsini si tu ilifanyika bila lengo lakini ilimaanisha makundi makundi hayo si tena makundi ya watu ya kawaida lakini inakuwa ni jumuiya inayolishwa kwa Mkate wa Mungu.

Yesu aliitwaa mikate na samaki wawili akiinua macho yake mbinguni, na kubariki. Papa anasema rejea ya tukio hili kwa Ekaristi ni dhahiri , kisha akaumenga mkate na kuwapa wanafunzi wake na wanafunzi wake waligawa mikate na samaki kwa watu wote bila kwisha. Walikula wote na kusaza. Hii inakuwa ni ishara ya Yesu , kuwa ndiye Mkate wa Mungu kwa Binadamu.

Wanafunzi wake waliona, lakini hawakuelewa ujumbe wake vizuri. Walimezwa na shauku za mshangao, jinsi ilivyowezekana kuulisha umati huo wa watu kwa mikate mitano na samaki wawili. Kwa mara ingine tena, wanafunzi walijawa na fikira za kibindamu na si zile za kimungu, kwamba , ujumbe mzima ni huduma, upendo na imani. Kwa muujiza huu, tunaapaswa kujifunza kwamba, Siku Kuu ya Mwili na Damu ya Kristu , hutualika sisi sote kuongekea imani katika matumaini , kushirikishana na kugwana kidogo kilichopo au kile tunachoweza kupata na wengine na kamwe tusijifungie kwa woga wa kuishiwa.
Papa alimalizia hotuba yake kwa kuomba msaada wa Mama Maria, atusaidie kuwa imara katika uongofu huu, na kweli kuwa wafuasi wa Yesu, tunaye mwabudu katika Ekaristi. Amina.








All the contents on this site are copyrighted ©.