2013-06-03 15:25:28

imepita miaka hamsini tangu alipofariki Papa Yohane XIII


Jumatatu hii, June 3, imetimia miaka hamsini kamili, tangu Mwenye Yohane XXIII, alipofariki duniani. Mwenye Heri Yohane XIII, kabla ya kuwa Papa aliitwa Angelo Giuseppe RONCALLI alifariki dunia Juni 3, 1963, ikiwa miezi miwili baada ya kukamilisha waraka wake maalum wa kichungaji juu ya Amani Duniani (Pacem in Terris).
Papa Yohana XIII, alichaguliwa kuwa Khalifa wa Kiti cha Petro tarehe 28 Oktoba 1958 katika umri wa miaka 77. Inaelezwa wakati wa kuchaguliwa kwake, wengi walimwona kama ni Papa mlezi... Lakini alishangaza wengi kwamba katika kipindi cha utawala wake wa miaka minne na nusu kama Papa na Askofu wa Roma, alizindua mengi kwa Kanisa Katoliki, moja wapo ikiwa ni kuitisha kwa Mkutano Mkuu wa Pili wa Vatican.










All the contents on this site are copyrighted ©.