2013-06-01 09:06:05

Katiba ni jambo tete lishughulikiwe kwa umakini mkubwa!


Askofu mkuu Paul Ruzoka , Mwenyekiti wa Tume ya haki na amani ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania katika mahojiano na Radio Vatican anabainisha kwamba, mchakato wa Katiba Mpya ya Tanzania ni jambo tete linalopaswa kushughulikiwa kwa umakini mkubwa. RealAudioMP3

Mchakato huu umekwishapitia hatua mbali mbali na Jumatatu, tarehe 3 Juni 2013, Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania itazindua Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Anasema, mchakato huu bado haujakidhi matakwa ya watanzania walio wengi ndiyo maana kumekuwepo na manung'uniko kadha wa kadha, kwani masuala ya kidini yameonekana kutawala zaidi, kinyume cha matarajio ya wengi. Kimsingi watanzania wengi wanataka Katiba ambayo itajenga na kuimarisha umoja, upendo na mshikamano wa kitaifa. Katiba ambayo kimsingi ni sheria mama, kamwe isiwe ni chombo cha kuwagawa wananchi wa Tanzania kwa misingi ya ukabila, udini au mahali anapotoka mtu!

Katiba inapaswa kuzingatia mafao ya wengi, utu na heshima ya binadamu. Iwe ni Katiba inayoleta tija kwa watanzania wote na wala si kwa ajili ya masilahi ya kundi fulani miongoni mwa Jamii ya Watanzania.







All the contents on this site are copyrighted ©.