2013-05-29 12:16:40

Mapadre wa Jimbo Katoliki Embu, wanahamasishwa kujenga ari na moyo wa kimissionari tayari kuhudumia Majimbo mengine hitaji!


Askofu Paul Kariuki Njiru wa Jimbo Katoliki Embu, Kenya, anawaalika Mapadre wa Jimbo nchini Kenya kujenga na kuimarisha ari na moyo wa kimissionari, tayari kujitosa bila ya kujibakiza kwa ajili ya kutangaza Habari Njema ya Wokovu katika maeneo ambayo yanakabiliwa na upungufu mkubwa wa wahudumu wa Injili na Mafumbo ya Kanisa.

Askofu Njiru ameyasema hayo Jumatatu tarehe 27 Mei 2013 wakati alipokuwa anazungumza kwenye mkutano wa Mapadre wa Jimbo Katoliki la Embu. Takwimu zinaonesha kwamba, kila Parokia ya Jimbo Katoliki Embu ina wastani wa Mapadre watatu wanaohudumia Parokia, wakati ambapo kuna baadhi ya Majimbo nchini Kenya, parokia zinahudumiwa na Padre mmoja au wakati mwingine hazina hapa Padre, hali inayowafanya waamini kuadhimisha Ibada bila Padre.

Jimbo Katoliki Embu linawahamasisha mapadre wake kujitoa kwenda Majimbo mengine kutangaza Habari Njema ya Wokovu kama alama ya mshikamano wa kichungaji na Majimbo ambayo bado yana upungufu wa wahudumu na wala si kwamba, Jimbo Katoliki la Embu lina Mapadre wengi zaidi. Hadi sasa kuna Mapadre wawili wanaotoa huduma ya kichungaji nje ya Jimbo hili.







All the contents on this site are copyrighted ©.