2013-05-28 10:54:20

Siku kuu ya Ekaristi Takatifu iwe ni fursa ya kuonesha imani ya Kanisa katika uwepo wa Mwili na Damu ya Kristo katika Sakramenti hii!


Katika Maadhimisho ya Sherehe ya Ekaristi Takatifu, Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi, tarehe 30 Mei 2013, Saa 1:00 za Usiku, anatarajiwa kuadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Yohane wa Laterano na baadaye kufuatia Maandamano ya Ekaristi Takatifu kuzunguka mitaa na viunga vya mji wa Roma.

Kardinali Agostino Vallini, Makamu Askofu Jimbo kuu la Roma anawakumbusha Mapadre na Waamini kwa jumla kwamba, Maadhimisho ya Sherehe ya Ekaristi Takatifu kwa Mwaka huu, yanabeba uzito wa pekee kwani yanafanyika katika Maadhimisho ya Mwaka wa Imani, changamoto kwa waamini kutolea ushuhuda wa imani yao kwa Kristo na Kanisa lake, wakionesha kwa namna ya pekee uwepo wa Kristo anaye andamana na wafuasi wake katika hija ya maisha yao ya kila siku. Ile ni nafasi kwa waamini kuonesha imani yao kwa uwepo wa Kristo katika Sakramenti ya Ekaristi Takatifu.

Kardinali Agostino Vallini anachukua fursa hii kuwaalika waamini kujitokeza kwa wingi ili kushiriki katika Ibada ya Misa Takatifu na baadaye katika Maandamano ya Ekaristi Takatifu.







All the contents on this site are copyrighted ©.