2013-05-25 12:12:21

Mwenyeheri Don Giuseppe Puglisi alisimama kidete kupambana na Kikundi cha Mafia hata akayamimina maisha yake kwa ujasiri mkuu!


Rais Giorgio Napolitano wa Italia amemwandikia barua Kardinali Paolo Romeo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Palermo, katika Maadhimisho ya Ibada ya kumtangaza Don Giuseppe Puglisi kuwa mwenyeheri. Rais Napolitano anasema kwamba, anaungana na wote wanaoadhimisha tukio hili la kihistoria ambalo Padre Puglisi alilionesha kwa njia ya ushuhuda wa maisha yake ya Kikristo, kiasi hata cha kuyamimina maisha kama kielelezo cha ukarimu na ujasiri wa hali ya juu.

Mauaji ya Don Puglisi yalisababisha majonzi na masikitiko makubwa miongoni mwa wananchi wa Italia, lakini bado kuna kumbu kumbu hai katika mawazo na mioyo ya wananchi wengi wa Italia kutokana na mchango wake mkubwa katika shughuli za kichungaji huko Sicilia. Ni kielelezo makini cha mtu ambaye amesimama kidete kupambana kufa na kupona na kikundi cha Mafia.

Itakumbukwa kwamba, Don Puglisi aliuwawa kikatili na Kikundi cha Mafia kutokana na chuki za kiimani hapo tarehe 15 Septemba 1993. Ametangazwa kuwa Mwenyeheri tarehe 25 Mei 2013.







All the contents on this site are copyrighted ©.