2013-05-24 15:16:07

Papa kutembelea Assisi 4 Ocktoba


Taarifa imetolewa kwamba, Papa Fransisko, atatembelea Assisi Oktoba 4 , 2013, ambayo NI Siku Kuu ya Mtakatifu Francis, mlezi wa Italia.
Askofu Mkuu wa Assisi-Nocera Umbra-Gualdo Tadino, Msgr. Domenico Sorrentino, ametangaza hilo, na kueleza kwamba, katika maadhmisho hayo, kengele ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Fransisko, litapigwa kwa muda mrefu, kama ishara ya kumshukuru Mungu kwa majaliwa ya Mungu na pia kama ishara ya furaha ya kutembelewa na Papa Fransisko.
Askofu Mkuu Sorrentino anasema, ziara hii ya Papa Fransisko kutembelea eneo lao, wanaipokea kuwa ni kitendo cha heshima na thamani sana, kitakacho ongeza nguvu ya kiroho kwa wakazi wa eneo hili. Itakuwa ni siku nzuri, ya tumaini na neema kubwa, kama ambavyo ni tayari anajionyesha kwa Kanisa zima, kwa njia ya ushuhuda wake wa maisha na maneno yake. Hii itakuwa zaidi kuwaimarisha Wafransiskano tu lakini pia kukutana watu maskini wa mji wa Assisi, ushahidi wazi Mtakatifu Francsisko wa Assisi.









All the contents on this site are copyrighted ©.