2013-05-24 09:00:29

Mafanikio ya Kijiji cha Matumaini, Jimboni Dodoma, Tanzania


Padre Vincent Boselli, Muasisi wa Kijiji cha Matumaini kinachomilikiwa na kuendeshwa na Masista Waabuduo Damu Takatifu ya Yesu, kilichoko Jimbo Katoliki Dodoma anasema, Kijiji cha Matumaini kimepata mafanikio makubwa katika utoaji wa huduma kwa watoto walioathirika na ugonjwa wa Ukimwi kanda ya Kati, nchini Tanzania. Katika kipindi cha zaidi ya miaka kumi, watoto waliofariki dunia ni kidogo sana, ikilinganishwa na hali halisi ya athari za ugonjwa wa Ukimwi. RealAudioMP3

Watoto wanaohudumiwa kwenye Kijiji cha Matumaini afya zao zimeendelea kuboreka na sasa wako Kidato cha Nne, wako kifua mbele wanajiandaa kufanya mitihani ya Kidato cha Nne kwa Mwaka 2013. Idadi ya watu wanaohudumiwa kwenye Kijiji cha Matumaini imeendelea kuongezeka maradufu, hii inatokana na ukweli kwamba, watu wanathamini na kupenda huduma ya tiba na kinga inayotolewa kwenye Kijiji cha Matumaini.

Huduma ya kuzuia maambukizi ya virusi vya Ukimwi kutoka kwa Mama mjamzito kwenda kwa Mtoto zinazidi kuboreka mwaka hadi mwaka, hadi sasa takwimu zinaonesha kwamba, kuna watoto 400 wamezaliwa na wanawake waliokuwa na Ukimwi, lakini watoto ni salama salimini. Kuna zaidi ya watu 2,900 wanaohudumiwa kwenye Kijiji cha Matumaini.







All the contents on this site are copyrighted ©.