2013-05-23 15:39:23

Rais wa El Salvador atembelea Vatican


Mapema Alhamis hii, katika ukumbi wa Kitume wa Vatican, Papa alikutana na Rais wa Jamhuri ya El Salvador Mheshimiwa Rais Carlos Mauricio Funes Cartagena. Na baadaye Rais huyo alikutana na Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu wa Jimbo, akifuatana na Askofu Mkuu Dominique Mamberti, Katibu wa Mahusiano na Marekani.
Wakati wa mazungumzo yao yaliyofanyika kaitka hali ya kirafiki na maelewano , walitazama zaidi mahusiano mazuri yaliyopo , kati ya Jimbo Takatifu na Jimbo la El Salvador. Na pia waliyatazama maisha ya mtumishi wa Mungu, aliyewahi Askofu Mkuu wa San Salvador, AskofuMkuu Oscar Arnulfo Romero y Galdàmez , na umuhimu wa shuhuda zake, kwa ajili ya taifa zima la an Salvador. .

Na walipongeza mchango Kanisa unaofanikisha maridhiano na uimarishaji wa amani, na pia kupitia maeneo ya huduma ya elimu, na miradi ya kutokomeza umaskini na uhalifu wa kupangwa. Na pia walitazama baadhi ya masuala ya kimaadili kama vile ulinzi wa maisha ya binadamu, ndoa na familia.
Papa amthibitisha Kardinali Vallini kuwa Vika Mkuu wa Jimbo la Roma.
Aidha mapema Asubuhi hii, ilitolewa barua ya Papa Fransisko iliyoandikwa kwa lugha ya Kilatini, inayo mthibitisha Kardinali AUGUSTINO VALLINI, kuwa Vika wa Jimbo la Roma.









All the contents on this site are copyrighted ©.