2013-05-22 15:24:37

Roho Mtakatifu: Ufunguo wa akili na mazuri...


Baba Mtakatifu Fransisko, katika katekesi yake kwa mahujaji na wageni, Jumatano hii, ameendelea kuitaza imani ya muumini kwa makini akisema," ndugu zangu wapendwa: katika katekesi yetu juu ya Imani, kwa sasa tunaingia katika kipengere cha Roho Mtakatifu kwa Kanisa moja, takatifu, katoliki na la kitume. Roho Mtakatifu anaye huisha na kuliongoza Kanisa na kila muumini aliye ndani ya kanisa kutekeleza agizo la Kristu la kuwafanya watu wote kuwa wanafunzi wake"..
Papa aliendelea kueleza kuwa, Roho Mtakatifu huifungua akili na mioyo katika kuuona uzuri na ukweli wa Injili. Roho mwenye kuvishinda vishawishi vya kuwa na ubinafsi na mgawanyiko, mwenye kujenga umoja, mshikamano, maridhiano na upendo. Roho mwenye kutia nguvu zinazohitajika katika kuwa na ushupavu wa kumshuhudia Kristu Mfufuka. Roho wa missioni na uinjilishaji.
Na kwamba, moto wa Roho Mtakatifu, ulimiminwa juu ya mitume siku ya Pentekoste, kama zawadi na jibu la kuomba kwa biidii. Roho Mtakatifu, jibu kwa Roho ya kina katika maombi, inakuwa daima ni nafsi ya uinjilishaji mpya na roho wa maisha yetu kama wakristo.
Papa alieleza na kusali ili kwamba kila siku waamini waruhusu Roho Mtakatifu kufanya kazi ndani mwao, akiifanya upya imani, na kuifungua mioyo na kuvuviwa na zawadi zake na kujitahidi kuwa ishara ya umoja na ushirika na Mungu katikati ya familia ya binadamu.
Baada ya homilia yake Papa aliwaalika wote kusali pamoja naye, kwa nia ya kuwaombea waathirika wa maafa yaliyotokea kibunga kilichotokea Oklahoma.Alisali ili kwamba, Bwana mwenyewe na amfariji kila mmoja wao, na hasa wazazi walio poteza watoto katika tukio hili la kutisha.
Pia aliwakaribisha mahujaji wanaozungumza Kiingereza-kutoka Uingereza, Ireland, India, Canada na Marekani. Na alitoa salaam zake za kipekee kwa mahujaji kutoka Jimbo Kuu la Hartford na Chama Cha Wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Kikatoliki ya Amerika.
Na mwisho aliwapa baraka zake za Kitume , kwa wao wenyewe na kwa familia zao, na zawadi pekee ya hekima na ya amani ya Roho Mtakatifu akisema, Mungu awabariki wote!








All the contents on this site are copyrighted ©.